Kuhusu CHUTCU

Historia na Uhai Wa Chama

Chama Kikuu cha Ushirika wa Tumbaku Chunya (CHUTCU LTD) ni muungano wa Vyama vya Ushirika vya Msingi vinavyolima zao la biashara la Tumbaku Chunya na Songwe pamoja na mazao ya chakula. Chama hiki kiliandikishwa katika Daftari la Serikali tarehe 20/09/2000 kwa matazamio na hatimaye kupata usajili wa kudumu tarehe 30/01/2003. Chama Kikuu mpaka sasa kina jumla ya Vyama wanachama hai 30 kutoka wilaya za Chunya na Songwe na Ofisi za Chama Kikuu zipo Chunya Mjini, Mkoa wa Mbeya.

Dira yetu

Dira ya CHUTCU Ltd ni kutoa huduma bora kwa vyama vya ushirika wanachama kwa kuongeza thamani ya mazao yanayozalishwa na vyama hivyo na kuhakikisha uboreshaji wa maendeleo ya kijamii na kiuchumi ya wanachama wao

Dhamira

Dhamira ya CHUTCU Ltd ni kuboresha huduma kwa vyama wanachama na kuhakikisha kuwa wanazalisha tumbaku yenye ubora wa juu ili kupata bei nzuri ya kuvutia kwa ajili ya maendeleo yao ya kiuchumi

Benki zetu

CHUTCU LTD mpaka sasa inafanya biashara ya taasisi za kifedha/benki nne (4) ambazo zinatoa mikopo kwa wakulima wa tumbaku waliopo katika Vyama vya Msingi (AMCOS) 30 katika Mkoa wa kitumbaku Chunya. Benki hizo ni;

  1. CRDB PLC
  2. AZANIA BANK
  3. NBC LIMITED
  4. NMB PLC

Ujenzi wa Kiwanda

CHUTCU Ltd katika kuunga mkono jitahada za serikali imejenga kiwanda chenye mitambo ya kusaga unga wa nafaka inayotokana na mahindi pamoja na kufunga mtambo wa kukamua mafuta ya alizeti ili kuongeza thamani ya mazao yanayolimwa na wakulima wilayani Chunya. Mradi huu mpaka kukamilika unatarajia kutumia kiasi cha shilingi 367,657,726.63 ambapo kiasi hiki kitahusisha Shilingi 74,000,000 ununuzi wa mtambo wa kusaga unga, na kiasi cha shilingi 29,960,000 ikiwa ni ununuzi wa mtambo wa kukamua mafuta ya alizeti. Mitambo yote hii miwili imenunuliwa SIDO (Shirika la Maendeleo ya Viwanda Vidogo) na gharama za ujenzi wa jengo ni shilingi 262,697,726.63.

Uongozi

Bodi ya CHUTCU LTD

S/N

JINA

WADHIFA

1

Sebastian Masika

Mwenyekiti

2

Elieza Fijaboh

Makamu

3

Alberto Kacheza

Mjumbe

4

Violet Kawemba

Mjumbe

5

Yona Chawene

Mjumbe

6

Isaya Daniel

Mjumbe

7

Epimarcus Sikumoja

Mjumbe

8

Thomas Mgalula

Mjumbe

 

MENEJIMENTI

S/N

JINA

WADHIFA

1

Christian Msigwa

Meneja Mkuu

2

Juma Nshinshi

Meneja Shughuli

3

Daniel Mpigasupi

Mkaguzi wa Ndani

4

Francisco Chidege

Mhasibu

 IDARA ZA MENEJIMENTI

  1. Idara ya Utawala
  2. Idara ya Uzalishaji na Masoko
  3. Idara ya Ukaguzi wa Ndani
  4. Idara ya Uhasibu